• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Vibali vya Ujenzi

KIBALI CHA UJENZI (BUILDING PERMIT)

 

TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI (BUILDING PERMIT)

 

 1. KIBALI CHA UJENZI

Kulingana na Sheria ya Serikali za Mitaa Sura 288 (Urban Authorities) act (Cap. 288) (Development control Regulations, 2008, Mwongozo wa utoaji wa vibali vya ujenzi, 2018, si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya :-

  •  Kutuma maombi kwa mamlaka ya mji husika.
  • Kuwasilisha michoro ya jengo na kumbukumbu husika.
  • Kupata kibali cha maandishi kinachoitwa Kibali cha Ujenzi.


2. KIBALI CHA AWALI:

  • Inashauriwa kupata kibali cha awali kabla ya kuomba kibali cha ujenzi.  Hivyo muendelezaji anatakiwa aandae mchoro wa awali (sketch plans scale) 1:00 1:200 akionyesha aina ya ujenzi atakaokusudia kufanya ili aweze kupata ridhaa ya kuendelea ha hatua za kuanzaa michoro ya mwisho.


Faida:

  • Kuokoa muda na gharama iwapo michoro ya mwisho itaonekana kuwa na dosari za kitaalam ambazo zitahitaji kufanyiwa marekebisho.
  • Kuwa na uhakika kuhusu mahitaji muhimu ya kuzingatiwa wakati michoro inaandaliwa.


3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KIBALI CHA UJENZI

  • Baada ya michoro kukamilika, iwasilishwe ikiwa kwenye majalada kwa namna ambayo inaweza kufunguliwa na kusomeka michoro hiyo iwasilishwe kama ifuatavyo:-
  • Seti tatu za michoro ya jengo (Architectural drawings scale 1:100 & 1:50)
  • Seti mbili za michoro ya vyuma structural drawings (scale 1:50) kwa majengo ya ghorofa.


4. MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI:

Michoro itakayoandaliwa inatakiwa ionyeshe mambo yafuatayo:-

  • Namna jengo litalavyokuwa ”sections elevation”, "foundation”, “roof plan”, “site plan”.
  • Ramani ya kiwanja (location plan)
  • Namba na eneo la kiwanja kilipo
  • Jina la mmilikaji ardhi inayohusika
  • Jina la mchoraji, ujuzi na anwani
  • Ukubwa wa kiwanja kwa mita za mita za mraba
  • Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba
  • Ujazo wa kiwanja (plot coverage).
  • Uwiano (Plot ratio)
  • Urefu wa jengo kwenda juu (Height)
  • Matumizi yanayokusudiwa
  • Idadi ya maegesho yatayokuwepo
  • Umbali wa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja (setbacks) na
  • Mfumo wa kutoa maji taka hadi kwenye mashimo, au bomba la maji taka


5. VIAMBATANISHO:

  • Fomu moja ya maombi iliyojazwa kwa usahihi.
  • Hati ya kumiliki kiwanja au barua ya toleo au fomu iliyojazwa ya sehemu zisizopimwa.
  • Kumbukumbu nyingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo,
  • Makabidhiano n.k.
  • Nakala za risiti ya kodi ya kiwanja na kodi ya majengo.
  • Mabadiliko ya matumizi ya ardhi.
  • Ramani ya kiwanja iliyosajiliwa.


6. HATUA ZINAZOFUATWA WAKATI WA KUCHUNGUZA MAOMBI YA KIBALI

Zinafuata ni hatua zinazofuatwa wakati wa kuchunguza michoro hiyo:-

Kuwasilisha michoro na kulipia gharama ya kibali cha ujenzi.

  • Uhakiki wa miliki
  • Kukaguliwa usanifu wa michoro
  • Kukagua kiwanja kinchokusudiwa kuendelezwa
  • Uchunguzi wa matumizi ya jengo na kuwepo kwa kiwanja katika ramani M/Miji (TP drawing)
  • Uchunguzi  wa Maafisa Afya
  • Uchunguzi wa  mipango ya uondoaji majitaka
  • Uchunguzi wa tahadhari za moto
  • Uchunguzi wa uimara wa jengo
  • Kuwasilisha kwenye kikao cha mipango Miji baada ya kukamilisha taratibu zote.
  • Hatimaye kuandika na kutoa kibali.


7. FAIDA ZA KUWA NA KIBALI CHA UJENZI

  • Kujenga nyumba ambayo imethibitishwa kitaalamu kuwa ni salama.
  • Kuwa na mazingira bora kwa kuwa na mji uliopangwa.
  • Kuepuka hasara na usumbufu unaoweza kutokea iwapo ujenzi umefanyika bila kibali ikiwa ni pamoja na kushtakiwa mahakamani kuvunjiwa na kulipa gharama za uvunjaji.
  • Kulipwa fidia iwapo jengo litabomolewa kwa sababu maalum.
  • Kuweza kupata mkopo kutoka Taasisi za fedha.


8. MUDA

  • Michoro itaidhinishwa ndani ya siku saba (7) toka mwombaji awasilishe maombi ya jengo la chini (mfuto). Na siku kumi nne (14) jengo la ghorofa. Aidha ndani ya muda huo mwombaji ataarifiwa sababu za michoro kutoidhinishwa kupata kibali cha ujenzi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • DC MAGALA AKABIDHI KIASI CHA SHILINGI MILLIONIMOJA SHULE YA MSINGI MWAMBANI.

    March 12, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.