• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Historia

1. UTANGULIZI 

1.1 TASWIRA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA NANYUMBU

Halmashauri ya wilaya ya Nanyumbu, ni moja kati ya Halmashauri tisa za mkoa wa Mtwara. Halmashauri hii ilianzishwa chini ya Sheria namba 7 ya mwaka 1982 ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) na kutangazwa rasmi katika Gazeti la Serikali Na. 190 la tarehe 01 Julai 2007. Makao makuu ya Wilaya yapo mji wa Mangaka ambao upo umbali wa kilomita 54 kutoka Masasi kwenye barabara ya Mtwara-Songea.

Asili ya wenyeji wa wilaya ya Nanyumbu ni makabila ya wamakua, wayao, na wamatambwe ambao huzungumza lugha zao za asili pamoja na Kiswahili.

1.2 MIPAKA YA ENEO

Wilaya hii iko kati ya latitudo 360 na 380 mashariki mwa Greenwich na latitudo 100 na 120 kusini mwa Ikweta. Nanyumbu inapakana na wilaya ya Nachingwea upande wa kaskazini, wilaya ya Masasi kwa upande wa mashariki, wilaya ya Tunduru upande wa magharibi na Jamhuri ya Msumbiji kwa upande wa kusini.

1.3 HALI YA HEWA

Hali ya hewa katika wilaya ya Nanyumbu ni joto la wastani ambalo ni 25 0C huku joto la juu likiwa 32 0C. Kipindi cha Desemba hadi Aprili, upepo unaojaa unyevunyevu kutoka Kaskazini-Mashariki huelekea Kusini Magharibi na kupelekea msimu wa mvua wenye joto na unyevunyevu. Aidha, kipindi cha Mei hadi Novemba, upepo kutoka Kusini Mashariki husababisha wilaya kuwa kavu, baridi na isiyo na unyevunyevu. Wilaya hupata mvua ya  wastani wa 832 mm ambayo hunyesha msimu mmoja kwa mwaka kuanzia mwezi Desemba hadi Aprili.

1.4 ENEO LA KIUTAWALA

Wilaya ya Nanyumbu ina tarafa nne za kiutawala ambazo ni Nakopi, Nanyumbu, Mangaka na Maratani pamoja na jimbo moja la uchaguzi (Jimbo la Nanyumbu). Wilaya imegawanywa katika kata 17, vijiji 93 vilivyosajiliwa na vijiji vidogo 526. Wilaya ya Nanyumbu ni kubwa kijiografia ikilinganishwa na halmashauri zingine za mkoa wa Mtwara kwani ina eneo la ukubwa wa kilomita za mraba 5,071.5. Ukubwa wake wa kijiografia ni asilimia 30 ya Mkoa mzima ambao una eneo la ardhi la kilomita za mraba 16,720.

Ugawaji wa eneo la ardhi katika wilaya ya Nanyumbu unaonesha kuwa, tarafa ya Nakopi inachukua sehemu kubwa ya eneo la ardhi ikiwa na kilomita za mraba 1665.7, ikifuatiwa na tarafa ya Nanyumbu yenye kilomita za mraba 1628. Tarafa ya Mangaka ina kilomita za mraba 1040.4 huku tarafa ya Maratani ina eneo la jumla ya kilomita 737.4 za mraba.

1.5 IDADI YA WATU

Kwa Mjibu wa Sensa ya Kitaifa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Wilaya ilikuwa na Jumla ya wakazi wapatao 204,323 ambao ni wanawake 104,625 na wanaume 99,698. 

1.6 SHUGHULI ZA KIUCHUMI

Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Wilaya ya Nanyumbu hujishughulisha na shughuli za kilimo kwa ajili ya chakula na biashara. Mazao ya biashara yanayolimwa ni korosho, ufuta, karanga, choroko na mbaazi. Mazao ya chakula ni mahindi, mpunga, muhogo, mtama, mbaazi, njugumawe, kunde na upupu. Aidha, baadhi ya wakazi hujishughulisha na uvuvi katika mto Ruvuma.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Muda za Watendaji wa Vituo vya Kupigia Kura kwa Ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 July 02, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • “Nanyumbu: Lango Jipya la Uwekezaji Kusini”

    June 25, 2025
  • DAS Kanyinda Apongeza Mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Nanyumbu

    June 21, 2025
  • RC Sawala Aipongeza Nanyumbu kwa Kupata Hati Safi ya CAG

    June 19, 2025
  • FUM Nanyumbu Yavunja Rekodi ya Mapato na Kuandika Historia Mpya ya Miradi

    June 18, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.