• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Mzigo mpya wa Bilioni 5.3 watua Nanyumbu Miradi ya Maji

Posted on: May 30th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Nayumbu Mhe. Mariam Khatibu Chaurembo akizungumza katika mkutano wa wadau wa maji Nanyumbu

Na, Lunanilo Ngela

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maji, imeipatia Wilaya ya Nanyumbu Shilingi 5,376,841,442.54 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji kwa mwaka wa Fedha 2022/2023.

Haya yamebainishwa katika mkutano wa wadau wa maji uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mapema leo Mei 30, 2023 ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Mariam Chaurembo na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, madiwani wa Halmashauri, vyama vya siasa, watumishi wa Umma, pamoja na jamii za watuma maji.

Mheshimiwa Chaurembo amempongeza Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mhandisi Simoni Mchucha, pamoja na watendaji wa Idara hiyo kwa kusimamia kikamilifu na kutekelezaji miradi mbalimbali ya maji kwa vijiji 59 kati ya 89 vinavyohudumiwa na RUWASA wilayani hapo. Aidha, amezitaka jumuiya za watumia maji kuhakikisha miradi hiyo ya maji inajiendesha, ikiwa ni pamoja na kusoma mapato na matumizi ya miradi kwa wananchi.    

Naye Kaimu Meneja wa RUWASA Nanyumbu Mhandisi Simon Mchucha, amewaeleza wajumbe kuwa, Bilioni 5.3 zilizotolewa na Serikali zinatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa maji Kamundi, Likokona II, Mitumbati – Chilunda pamoja na upanuzi na ukarabati wa bwawa la maji Sengenya. Aidha, utafiti wa maji na uchimbaji wa visima sita unafanyika vijiji vya Mkwajuni, Chihuve, Rukumbi, Lumesule, Mpombe na Mbangala Mbuyuni.

Mhandisi Mchucha ameongeza kuwa, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 shilingi 2,086,419,158.00 zitatumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maji ikiwemo; Ujenzi wa Mradi wa Maji Mburusa na Michiga, ukarabati wa mradi wa maji Ndwika, Holola na Chivilikiti, uboreshaji wa mradi wa maji Mtawatawa na Nakopi.

Aidha, katika bajeti hiyo ya 2023/2024 visima kumi vitachimbwa kwa ajili ya utafutaji wa vyanzo vya maji katika vijiji vya Mtalikachau, Chipuputa, Lukwika, Mnanje A, Marumba, Namarupi, Mchenjeuka, Namaka, Nanderu na Nahawara.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Nanyumbu Cde. Rashid Mrope amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyopeleka fedha nyingi wilayani hapo kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Serikali ya awamu ya sita imeshaanza utekelezaji wa mradi kubwa wa kimkakati wa maji toka mto Ruvuma Kwenda Mangaka unaogharimu shilingi Bilioni 38.7 kupitia mkandarasi M/S AFCONS INFRASTRUCTURE LTD pamoja na Mtaalam Mshauri WAPCOS LTD.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.