• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Mkoa wa Mtwara waadhimisha Wiki ya Maji Nanyumbu

Posted on: March 24th, 2023


Katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed akizungumza na wanachi wa kijiji cha Mitumbati wilayani Nanyumbu

Na, Lunanilo Ngela

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed amezindua mradi wa maji wa Mitumbati-Chilunda wilayani Nanyumbu wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.35 zilizotokana na Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 pamoja na Programu ya PforR unaolenga kutatua kabisa tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika vijiji vya Mitumbati na Chilunda.

Akizindua mradi huo katika maadhimisho ya Wiki ya Maji ambayo kimkoa imefanyika wilayani Nanyumbu, Mkuu wa Mkoa amesema kuwa mradi wa Mitumbati-Chilunda ni moja kati ya miradi mingi ya maji iliyotekelezwa mkoani Mtwara katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan. Aidha, Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi kutunza miundombinu ya maji kwa kushirikiana na mamlaka za maji, kutunza vyanzo vya maji ikiwa ni pamoja na kuheshimu mipaka iliyowekwa ili kulinda vyanzo hivyo vya maji.

Katika maadhimisho hayo, Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed aliambatana na wakuu wa Wilaya nne za Mkoa wa Mtwara akiwepo Mkuu wa Wilaya mwenyeji Mhe. Mariam Khatibu Chaurembo, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Lauter John Kanoni, Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Kanali Patrick Kenan Sawala pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajabu Kundya.

Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Mariam Chaurembo akizungumzia suala la upatikanaji wa maji wilayani Nanyumbu amesema kuwa, pamoja na Serikali kutekeleza Mradi wa Mitumbati-Chilunda pia Serikali inatarajia kutekeleza mradi mkubwa wa Maji kutoka mto Ruvuma wenye thamani ya shilingi Bilioni 40. Miradi mingine inayotekelezwa wilayani Nanyumbu ni pamoja na mradi wa ukarabati na utanuzi wa bwawa la Sengenya unaogharimu shilingi Bilioni 3.6, Ujenzi wa bwawa la Maratani wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.2 na uchimbaji wa visima 10 vyenye thamani ya shilingi milioni 480 ambao umeshakamilika.

Maadhimisho ya Wiki ya Maji nchini hufanyika Machi 22 kila mwaka ikiwa ni utekelezaji wa Azimio Na. 47/193 la Umoja wa Mataifa (UN) linalolengo kuunganisha mataifa katika kutathimini utekelezaji, mafanikio na changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi ya maji. Aidha, azimio hili huyafanya mataifa kuainisha mikakati ya kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira na kusimamia utunzaji wa rasilimali ya maji.

Kauli Mbiu ya Wiki ya Maji kwa Mwaka 2023 ni “Kuongeza Kasi ya Mabadiliko katika Sekta ya Maji kwa Maendeleo Endelevu ya Kiuchumi”

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akikagua tanki la maji kwenye mradi wa Mitumbati-Chilunda

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Kanali Patrick Sawala (wa kwanza kulia), Mhe. Mwangi Kundya Mkuu wa Wilaya ya Newala (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Lauter Kanoni (wa nne kutoka kulia) wakiwa katika mradi wa maji


Mkuu wa Mkoa akifungua jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Mitumbati-Chilunda

Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nanyumbu Mhandisi Simon S. Mchucha akielezea hatua mbalimbali za utekelezaji wa Mradi mbele ya Mkuu wa Mkoa (wa pili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe Mariam Chaurembo (wa kwanza kushoto) na viongozi wengine walioshiriki maadhimisho hayo

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Kushoto kwa Mkuu wa Mkoa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nanyumbu Ndg. Ibrahim J. Mwanauta 

Mkuu wa mkoa wa Mtwara (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mwekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mtwara (wa pili kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Benjamin Masimbo (wa kwanza kulia)

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.