• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Ziara ya Rais Samia yashusha neema Nanyumbu

Posted on: September 17th, 2023

Na; Lunanilo Ngela

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mapema leo Septemba 17, 2023 amefanya ziara ya kikazi Wilaya ya Nanyumbu kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi.

Katika ziara hiyo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua ghala na miundombinu ya Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu (TANIPAC) wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.1 katika eneo la Naishero Kata ya Mangaka.

Rais Samia amezungumza na maelfu ya wananchi waliojitokeza kumpokea mjini Mangaka ikiwa ni pamoja na kupokea na kutatua kero za wananchi hao zilizowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu Mhe. Yahya Ally Mhata.

Naye Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Salvio Kapinga akitoa majibu ya utatuzi wa kero ya kukatika katika kwa umeme Nanyumbu amewaeleza wananchi kuwa, Rais Samia ametoa fedha za kutekeleza mradi wa Gridi Imara Songea - Masasi huku awamu ya pili (phase II) inayogharimu Bilioni 200 ikihusisha ujenzi wa njia (line) na vituo vya kupoozea umeme Tunduru – Masasi mradi ambao tayari umeshaanza.

Rais Samia ameipatia Wilaya ya Nanyumbu gari tatu za kubebea wagonjwa (ambulance) ili kuboresha upatikaji wa huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuwahakikishia wananchi hao juu ya uhakika wa soko la mazao ikiwemo mbaazi na ufuta.

Wananchi wa Wilaya ya Nanyumbu kupitia Mbunge wa Jimbo Mhe. Yahya Ally Mhata wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa dhamira yake ya dhati inayolenga kumaliza kabisa kero  ya uhaba wa maji Nanyumbu kwa kutoa mabilioni ya fedha ikiwemo Bilioni  38 za mradi wa maji Ruvuma, Bilioni 3.6 Mradi wa Maji Sengenya na Bilioni 3.2 mradi wa maji Maratani.

Aidha, wananchi hao wametoa shukrani kwa fedha za miradi mingine ya maendeleo ikiwemo Elimu, Afya, Miundombinu ya Umeme na Barabara zilizotolewa na Rais Samia kwa awamu tofauti tofauti ili kuboresha huduma za jamii.

Rais Samia leo Septemba 17, 2023 anahitimisha ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara iliyoanza Septemba 14, 2023.


 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.