• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Complaints |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • List of Leaders
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Stategies
  • Administration
    • Muundo
    • Idara
      • Water
      • Kilimo
      • Finance and Accountants
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali yatatua mgogoro hifadhi ya msitu Mbangara wilayani Nanyumbu

Posted on: December 28th, 2022

Katika picha ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri nane wa Kisekta Mhe. Dr. Angeline Sylvester Mabula (katikati) akiwasili katika kijiji cha Wanika

Na, Lunanilo Ngela

Serikali kupitia Kamati ya Mawaziri nane wa Kisekta ikiongozwa na Mhe. Dr. Angeline Mabula (Mb) ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imekutana na wananchi wa vitongoji vya Livambangoma, Wanika, Namaromba na Nambunda wilayani Nanyumbu wanaoishi kwenye hifadhi ya msitu Mbangara na kuwatengenezea mpango wa makazi mapya wananchi hao ili kupisha eneo la hifadhi.

Akizungumza na wananchi hao Mhe. Dr. Mabula amesema kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ikishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu itaandaa utaratibu mzuri wa kuwagawia maeneo wananchi hao katika vijiji mama yaani Mbangara Mbuyuni na Marumba. Aidha, ameongeza kuwa serikali itahakikisha zoezi hilo linafanyika kwa utulivu na kila mwananchi anatendewa haki.

Katika ziara hiyo Mhe. Mabula aliongozana na  Mhe. Balozi, Dr. Pindi Chana (Mb) Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Anthony Mavunde (Mb) Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Maryprisca Mahundi (Mb) Naibu Waziri wa Maji na Mhe. Khamis Hamza Khamis (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali. Ahmed Abbas Ahmed akizungumza na wanachi hao amesema kuwa Serikali ina mpango mzuri wa matumizi ya ardhi na hivyo kuwataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikiwaandalia wananchi hao uratatibu wa makazi. Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Marium Chaurembo ameishukuru Serikali chini ya Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuipatia Nanyumbu Miradi ya maendeleo ikiwemo Mradi wa maji wa mto Ruvuma. Aidha, mbunge wa Jimbo la Nanyumbu Mhe. Yahya Ally Mhata ameiomba Serikali kuendelea kushirikiana na wananchi wa vijiji hivyo kwani wana mchango mkubwa katika shughuli za maendeleo nchini.  


Matangazo

  • Tangazo la Kazi za Muda za MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 May 06, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA NANYUMBU July 02, 2022
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Baraza la Madiwani lapokea na kujadili Taarifa ya Maendeleo ya Kata 17 Nanyumbu

    January 26, 2023
  • Tarifa kwa Umma

    January 25, 2023
  • Tarifa kwa Umma

    January 25, 2023
  • Serikali yatatua mgogoro hifadhi ya msitu Mbangara wilayani Nanyumbu

    December 28, 2022
  • Ona yote

Video

Utalii wa ndani Nanyumbu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • miongozo

Tovuti Mashuhuri

  • Public Service Management
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2017 Nanyumbu Distict Council . All rights reserved.