• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Nanyumbu wapongezwa kwa mikakati bora ya elimu

Posted on: July 13th, 2017

Nanyumbu wapongezwa kwa mikakati bora ya elimu

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Halima Dendego akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kabati za kuhifadhia vifaa vya maabara Shule ya Sekondari Mikangaula wakati ziara yake inayoendelea wilayani hapa

 


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego amepongeza juhudi kubwa zinazofanywa na uongozi wa Wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu katika kutatua changamoto za Elimu. Akizungumza kwa nyakati tofauti katika ziara yake ya kikazi inayoendelea hapa Wilayani Nanyumbu amesema uongozi wa Wilaya ya Nanyumbu ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mheshimiwa Joackim Wangabo pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Hamis Dambaya umemkabidhi mpango mkakati ambao unatekelezeka kwa vitendo.

Amesema kwa muda mrefu wilaya ya Nanyumbu imekuwa ikinyooshewa vidole kwa kuwa na matokeo mabaya ya mitihani kwa wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari.  Amesema mpango mkakati aliokabidhiwa na hali halisi anayoiona kwa vitendo ni ushahidi tosha kwamba Nanyumbu sasa inakimbia katika maendeleo.

Amesema kwa muda mrefu vyombo vya habari akiwemo ‘Mwewe’ wa Cloudz TV wamekuwa wakitembelea na kuripoti changamoto nyingi za wilaya hii. Amesema ni jambo jema kwani linawaamusha na kuwakumbusha kutimiza wajibu wao. Aidha, amemtaka Mwewe arudi Nanyumbu ili kujionea mabadiliko yaliyopo sasa.

Hata hivyo Mheshimiwa Dendego amesikitishwa na mimba za wanafunzi na kutangaza mapambano makubwa na wanafunzi wanaopata ujauzito. Amesema taarifa zinaonesha mwaka 2016 jumla ya wanafunzi 22 wilayani Nanyumbu walipata ujauzito. Amesisitiza kuwa suala hilo halikubaliki kwani linadumaza maendeleo.

Amesema mwanafunzi anayepata ujauzito ni mtuhumiwa namba moja. Aidha amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo kuhakikisha anamfikisha kwenye vyombo vya sheria mwanafunzi yeyote anayepata ujauzito shuleni. Amesema watoto wa kike wamekuwa sababu mojawapo ya ushawishi wa kupata mimba kwa kuvaa nguo zinazoshawishi zinaa, pia vitendo vya kuwavutia wavulana.

Amesema maelekezo yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais ya kuzuia wanafunzi wanaopata ujauzito kurudi shule kwa mfumo wa kawaida ni sahihi na yeye mwenyewe yuko tayari kuyasimamia. Amewataka wananchi na makundi ya kijamii yanayopiga kelele kupinga hatua hiyo yaache mara moja.

Licha ya kuwataka wanafunzi wa Nanyumbu kubadilika Mheshimiwa Dendego ametoa michango mbalimbali katika sekta ya Elimu ambapo amechangia mifuko ya saruji 50 katika shule ya Msingi Lidede na kuahidi kugharamia mbao za milango na madilirisha katika shule hiyo.

Awali akiwasilisha mpango mkakati wa Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Hiyo, Hamis Dambaya amesema kuwa kwa kutambua changamoto kubwa ya elimu katika halmashauri hii wameamua na wamejipanga katika miakakati imara inayotekelezeaka.

Moja ya mikakati hiyo ni pamoja na kuwatumia wananchi ambao wamehamasika na kuitambua falsafa ya uchangiaji wa elimu. Amesema kutokana na uhaba wa fedha katika utekelezaji wa malengo waliojiwekea wananchi wamehamasika kutumia nguvu zao katika kufyatua tofali kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo. Aidha katika mwaka wa fedha wa 2017/2018 Halmashauri imetenga shilingin 250,000,000 kupitia fedha za maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika shule za msingi Mikuva, Michiga B, Nanderu, Nandete na Nakatete. Kwa sasa wilaya hiyo ina upungufu wa vyumba vya madarasa 254 sawa na asilimia 50. Wakati ujenzi wa nyumba za walimu umefikia asilia 63.

Mikakati mingine ni kuongeza uwezo wa idara ya Uthibiti wa ubora wa elimu katika kukagua shule ambapo wamekuwa wakisaidia kwa huduma ndogondogo ikiwemo usafiri kuzifikia shule husika.

Kwa upande wa wananchi wa Nanyumbu wamepongeza Mheshimiwa Dendego kwa kuthamini jitihada zao na kumtaka aendelee kuwabana wazazi wasiojiheshimu.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mikangaula, Said Mkareha amemtaka Mheshimiwa Dendego aendelee kupambana. Pia awabane wazazi wanaovaa nguo zisizo stahili kwani ni moja ya vishawishi vya zinaa.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.