• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Dkt.Leonard Akwilapo akikagua moja ya mabanda ya maonesho wakati wa kilele cha maazimisho ya wiki ya Elimu Kitaifa tukio lililoadhimishwa Mkoani Mtwara Tarehe 28/04/2017

Posted on: April 28th, 2017

Katibu Mkuu awataka Wadau wa Elimu kushirikiana kutatua changamoto za elimu Nchini.


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Dkt.Leonard Akwilapo amewataka wadau wote wa elimu kuwa sehemu ya utatuzi wa changamoto za elimu hapa nchini. Hayo amesema jana wakati akifunga Juma la Elimu Kitaifa lililofanyika shule ya Sekondari Mangaka iliyoko Wilayani Nanyumbu mkoani Mtwara.

Dkt. Akwilapo amesema changamoto za elimu ni nyingi hivyo zinapaswa kutatuliwa kwa ushirikiano wa kila mdau. Ameyataja baadhi ya masuala muhimu yanayopaswa kupewa kipaumbele kwa kipindi hiki kuwa ni pamoja na uimarishaji na usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji ambapo Walimu, Wadhibiti Ubora wa Elimu, Viongozi wa Halmashauri na wadau wote wa Elimu wanapaswa kuhakikisha wanatumia nafasi zao kuondoa changamoto hizo.

Katika sherehe hizo zilizoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) Akwilapo amesema kwa sasa ufaulu wa shule zisizo za serikali hapa nchini zinaongoza. Siri kubwa ya ufaulu huo ni usimamizi mzuri jambo ambalo hata serikali inaweza iwapo kila mdau ataamua kuwajibika katika sehemu yake.

‘Kama serikali tunapaswa kuangalia na kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi. Walimu wanaofundisha serikalini na shule za binafsi ni walewale na wamesoma vyuo vilevile, lakini wanapoenda shule binafsi wanafanya vizuri. Kwa nini wasifanye vizuri hata wanapokuwa katika shule za serikali’? Amesema Akwilapo.

Aidha, Dkt. Akwilapo amekemea tabia ya baadhi ya walimu kufanya kazi binafsi nyakati za masomo wakiwemo wale wanaoendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda. Amesema hiyo ni moja ya sababu zinazokwamisha maendeleo ya elimu hapa nchini. Amewataka Wadhibiti ubora wa shule waboreshe njia za kufanya tathimini. Badala ya kuanza kutoa taarifa kwa walimu kabla ya kwenda kuwakagua, wawe na utaratibu wa kuvamia ili kuwabaini walimu wanaotoka kwenye vituo vyao vya kazi kabla ya wakati. Hilo litasaidia kuwafanya walimu wawe tayari muda wote.

Pia wadhibiti ubora wawe na kumbukumbu ya watu waliokwisha wakagua badala ya kujikuta wanamkagua mwalimu mmoja tu kila wanapotembelea shule husika.

Kwa upande wake Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Kathleen Sekwao amemtaka Katibu Mkuu kuhakikisha mkoa wa Mtwara na hasa wilaya ya Nanyumbu inaangaliwa kwa jicho la pekee ili kutatua changamoto nyingi zilizopo. Amesema wao kwa upande wao watahakikisha wanautangaza mkoa kwa wadau mbalimbali ili wasaidiane na wenyeji katika kuinua kiwango cha elimu.

Pia ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kutatua changamoto mbalimbali za elimu kama vile kuongeza bajeti kulinganna na mahitaji yakiwemo mahitaji ya watoto wenye mahitaji maalumu. Na kutoa motisha kwa walimu wanaofanya kazi katika mazingira magumu.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.