• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

DC Chaurembo ayashauri Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali Nanyumbu kushirikisha wataalam wa Halmashauri uandishi wa maandiko ya miradi

Posted on: May 25th, 2023

Viongozi wa Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali wilayani Nanyumbu wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya Mhe. Mariam Chaurembo (aliyekaa katikati)

Na, Lunanilo Ngela

Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Mariam Khatibu Chaurembo amewataka watendaji wa Halmashauri kutoa ushirikiano wa kitaalam katika uandishi wa maandiko ya miradi kwa Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali yaliyopo wilayani Nanyumbu pindi unapohitajika ili kuyawezesha mashirika hayo kupata fedha za miradi yenye tija kwa maendeleo ya jamii.

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa ushauri huo mapema leo Mei 25, 2023 katika Mkutano wa mwaka wa Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali Nanyumbu, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri na kuhudhuriwa na watumishi mbalimbali wa umma pamoja na viongozi wa mashirika saba yasiyokuwa ya kiserikali yaliyomo wilayani humo.

Viongozi wa mashirika hayo wamweleza Mkuu wa Wilaya kuwa, changamoto kubwa inayowakabili ni kukosekana kwa fedha za wafadhili huku baadhi ya maandiko yao ya miradi yakikosa vigezo, na hivyo Mkuu wa Wilaya kuwataka wataalam wa Halmashauri, kutoa ushirikiano wa kitaalam katika uandishi wa maandiko ya miradi kwa mashirika hayo yenye mchango mkubwa katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo ujenzi wa miundombinu.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Nanyumbu Ndg. Salum Abdul Palango pamoja na Mwakilishi wa Mkurugenzi ambaye pia ni Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Ndg. Philipo Sengela, wameahidi kuwa wataendelea kutoa ushirikiano kwa mashirika hayo ambayo yapo kisheria na kusimamiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002, iliyofanyiwa marekebisho na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Juni, 2005 kupitia Sheria ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali Na. 11 ya mwaka 2005, na Sheria Na. 3 ya mwaka 2019, inatoa tafsiri ya Shirika Lisilo la Kiserikali kuwa ni “Kikundi binafsi na cha hiari cha watu au mashirika, kisicho cha kisiasa wala kidini, kisicho cha kugawana faida, ambacho kimeundwa katika ngazi ya jamii kitaifa na kimataifa, chenye dhamira ya kukuza malengo halali ya kiuchumi, kijamii au kiutamaduni, kuhifadhi mazingira, kulinda na kutetea haki za binadamu na utawala bora katika jamii”.

Wilayani Nanyumbu Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali yamejipambanua kujikita katika masuala yahusuyo afya, elimu, Michezo, msaada wa kisheria, utetezi wa haki za watoto, pamoja na shughuli za kilimo. Aidha, utekelezaji wa miradi hiyo hutegemea zaidi fedha za wafadhili.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili June 11, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • RC Sawala Apongeza Ujenzi wa Shule ya Sekondari Kilimanihewa, Awataka Wananchi Kuendeleza Ushirikiano

    June 11, 2025
  • DC Magala Afungua Mafunzo ya Jeshi la Akiba Nanyumbu

    June 10, 2025
  • "Tutachukua Hatua Kali kwa Watakaohujumu Wakulima" DC Magala

    June 09, 2025
  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.