• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Complaints |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • List of Leaders
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Stategies
  • Administration
    • Muundo
    • Idara
      • Water
      • Kilimo
      • Finance and Accountants
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Chaurembo afungua Kongamano la ushawishi wa ushiriki wa viziwi katika masuala ya afya Nanyumbu

Posted on: March 4th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Mariam Khatibu Chaurembo akizungumza na washiriki wa kongamano

Na, Lunanilo Ngela

Akifungua kongamano hilo la “Ushawishi Kuhusu Ushiriki wa Viziwi katika Masuala ya Afya” lililoandaliwa na Chama cha Viziwi (CHAVITA) Mkoa wa Mtwara na kudhaminiwa na Abilis Foundation, Mkuu wa Wilaya amesema kuwa  huduma za afya ni haki ya kila mwanajamii na kwamba lengo la serikali ni kuhakikisha kila mwananchi anapatiwa huduma bora za kiafya.

Mheshimiwa Chaurembo amewapongeza CHAVITA kwa kuendesha mafunzo ya siku mbili kwa washiriki yaliyolenga kuwajengea uwezo katika nyanja mbalimbali ikiwemo masuala ya afya ya uzazi pamoja na haki za uzazi kwa wanawake viziwi. Aidha, amewataka washiriki wa mafunzo hayo kujikita katika shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujiongezea kipato ikiwa ni pamoja na kuomba mikopo isiyo na riba inayotolewa na Halmashauri kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

Mwenyekiti wa CHAVITA Mkoa wa Mtwara Bi. Farida Selemani amemshukuru Mkuu wa Wilaya na watendaji wengine wilayani Nanyumbu kwa kushiriki kongamano hilo na kuuomba uongozi wa Wilaya kushirikiana bega kwa bega na watu wenye ulemavu ikiwemo viziwi katika masuala mbalimbali mhimu ili kurahisisha upatikanaji wa haki za makundi hayo maalum.

Shughuli zilizofanywa na CHAVITA Nanyumbu katika mradi wa awamu hii ni mafunzo ya siku mbili yahusuyo afya kuanzia tarehe 02 – 03/03/2023 pamoja na kongamano la tarehe 04/03/2023 alisema Mratibu wa Miradi CHAVITA Mkoa Ndg. Kasim Mchindula. Aidha, mratibu huyo aliongeza kuwa matokeo yanayotarajiwa baada ya mafunzo ni pamoja na ushiriki na ushirikishwaji wa viziwi katika msuala mbalimbali yahusuyo afya.


Matangazo

  • Tangazo la Kazi za Muda za MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 May 06, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA NANYUMBU July 02, 2022
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Karibuni Nanyumbu waajiriwa wapya Divisheni za Afya na Elimu

    June 06, 2023
  • Motisha ya Milioni 18.2 yatolewa kwa Walimu na Wanafunzi Nanyumbu

    June 05, 2023
  • Serikali yaipatia Nanyumbu Bilioni 3 Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana

    June 01, 2023
  • Mzigo mpya wa Bilioni 5.3 watua Nanyumbu Miradi ya Maji

    May 30, 2023
  • Ona yote

Video

Utalii wa ndani Nanyumbu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • miongozo

Tovuti Mashuhuri

  • Public Service Management
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2017 Nanyumbu Distict Council . All rights reserved.