• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Maadili ya Msingi
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo
    • Divisheni
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Industry, Trade and Investments
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Planning and Coordination
      • Human Resource Management and Administration
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Natural Resources and Environment Conservation
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Biashara
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Information and Communication Technology
      • Government Communication
    • Wards
      • Chipuputa
      • Mangaka
      • Kilimanihewa
      • Sengenya
      • Kamundi
      • Maratani
      • Nandete
      • Nanyumbu
      • Mkonona
      • Masuguru
      • Likokona
      • Michiga
      • Napacho
      • Lumesule
      • Mnanje
      • Mikangaula
      • Nangomba
    • Villages
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Utalii
      • Hifadhi ya Wanyama ya Lukwika Lumesule
      • Daraja la Mtambaswala
      • Sehemu za Kiutamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
    • Elimu
      • Ujenzi wa Vyuo Vikuu
      • Ujenzi wa Vyuo vya Kati
      • Ujenzi wa Shule Binafsi
    • Maeneo ya Viwanda
    • Ujenzi wa Mahoteli
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Watumishi
    • Ujasiriamali
    • Biashara
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM)
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma

CCM kumaliza kabisa kero ya maji Nanyumbu

Posted on: September 14th, 2020

Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Ndg. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nanyumbu


Na, Lunanilo L. Ngela

Akiwa katika Mji wa Mangaka Ndg. Samia Suluhu Hassan, amewaeleza wananchi dhamira ya Chama Cha Mapinduzi ya kumaliza kabisa kero ya maji wilayani Nanyumbu kupitia Mradi Mkubwa wa maji wa Mto Ruvuma. Usanifu wa Mradi huo umekamilika.

Pamoja na Mradi huo, Serikali katika kutekeleza ilani ya CCM ya 2015-2020 imetekeleza miradi mbalimbali ya maji wilayani Nanyumbu ukiwepo Mradi wa maji Nandete unaogharimu Shilingi milioni 285.499. Miradi ya maji ya lipa kulingana na matokeo (P4R) yenye thamani ya Bilioni 1.3 ipo hatua mbalimbali katika vijiji vya Nangomba/Mjimwema, Mkwajuni/Mikangaula na Kisimatuli/Masyelele. Aidha, Ujenzi wa bwawa la maji Maratani unaogharimu bilioni 1.4 unaendelea.

Akizungumzia Huduma za Afya, Ndg. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi katika Ilani yake ya 2020-2025 kitaendelea kuboresha huduma za Afya kwa kuongeza hospitali 98 za Halmashauri nchini, hospitali 10 za Rufaa ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za Bima ya Afya.

Mwaka 2015-2020 wilayani Nanyumbu umefanyika Ujenzi wa Kituo cha Afya Mtambaswala unaogharimu shilingi milioni 400, Ujenzi wa wodi wa wazazi Hospitali ya Mangaka Milioni 400, Ujenzi wa Jengo la mionzi (X-Ray) hospitali ya Wilaya ikiwa ni pamoja na Ujenzi unaoendelea wa Kituo cha Afya Mikangaula unaogharimu milioni 200.

Chama cha Mapinduzi kupitia Mgombea mwenza kimeahidi kuwa ikiwa kitapata ridhaa ya kuongoza nchi kwa miaka mitano tena kitaendelea na sera yake ya Elimu bure ili kuhakikisha wanafunzi wanapata haki yao ya kimsingi ya Elimu.

Ifikapo 2023 Tanzania yote itakuwa na umeme, alisema Ndg. Samia Suluhu Hassani akizungumzia Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijiji ambao upo hatua ya tatu (REA III).

Akizungumzia suala la miundombinu ya barabara Mjini Mangaka, Ndg. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa ujenzi wa lami kilomita saba utatekelezwa. Aidha, Wakala wa barabara mijini na vijijini (TARULA) itaendelea kuongezewa bajeti ili kuimarisha miundombinu ya barabara.

Mgombea Ubunge Jimbo la Nanyumbu Ndg. Yahya Ally Mhata pamoja na wagombea udiwani wa Kata za Kilimanihewa na Mangaka kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi wameelezea namna Serikali inayosimamiwa na CCM ilivyotekeleza Miradi mikubwa Nanyumbu ukiwemo mradi mkubwa wa kimkati wa Ujenzi wa Stendi ya Kisasa ya Mabasi Mangaka unaogharimu Shilingi Bilioni 2.1. Aidha, Wagombea hao wameomba wananchi kuwachagua katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28/10/2020.    



Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendeshaji Vifaa vya Bayometriki January 23, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi August 09, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji September 16, 2024
  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 September 26, 2024
  • Ona yote

Habari Mpya

  • Nanyumbu Yang’ara Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025

    May 17, 2025
  • Afisa Mwandikishaji Nanyumbu Awataka Washiriki wa Mafunzo Kuhakikisha Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura Linatekelezwa kwa Ufanisi

    May 14, 2025
  • DC MAGALA AWAASA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CWT NANYUMBU KUCHAGUA VIONGOZI BORA NA SIO BORA VIONGOZI.

    March 19, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA WA MTWARA YAFANYA ZIARA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE NANYUMBU.

    March 17, 2025
  • Ona yote

Video

Kituo cha mabasi Mangaka
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HUDUMA ZA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • UTALII NANYUMBU

Tovuti Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Haki Zote Zimehifadhiwa.