• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Complaints |
Nanyumbu District Council
Nanyumbu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • List of Leaders
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Stategies
  • Administration
    • Muundo
    • Idara
      • Water
      • Kilimo
      • Finance and Accountants
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CCM kumaliza kabisa kero ya maji Nanyumbu

Posted on: September 14th, 2020

Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Ndg. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nanyumbu


Na, Lunanilo L. Ngela

Akiwa katika Mji wa Mangaka Ndg. Samia Suluhu Hassan, amewaeleza wananchi dhamira ya Chama Cha Mapinduzi ya kumaliza kabisa kero ya maji wilayani Nanyumbu kupitia Mradi Mkubwa wa maji wa Mto Ruvuma. Usanifu wa Mradi huo umekamilika.

Pamoja na Mradi huo, Serikali katika kutekeleza ilani ya CCM ya 2015-2020 imetekeleza miradi mbalimbali ya maji wilayani Nanyumbu ukiwepo Mradi wa maji Nandete unaogharimu Shilingi milioni 285.499. Miradi ya maji ya lipa kulingana na matokeo (P4R) yenye thamani ya Bilioni 1.3 ipo hatua mbalimbali katika vijiji vya Nangomba/Mjimwema, Mkwajuni/Mikangaula na Kisimatuli/Masyelele. Aidha, Ujenzi wa bwawa la maji Maratani unaogharimu bilioni 1.4 unaendelea.

Akizungumzia Huduma za Afya, Ndg. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi katika Ilani yake ya 2020-2025 kitaendelea kuboresha huduma za Afya kwa kuongeza hospitali 98 za Halmashauri nchini, hospitali 10 za Rufaa ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za Bima ya Afya.

Mwaka 2015-2020 wilayani Nanyumbu umefanyika Ujenzi wa Kituo cha Afya Mtambaswala unaogharimu shilingi milioni 400, Ujenzi wa wodi wa wazazi Hospitali ya Mangaka Milioni 400, Ujenzi wa Jengo la mionzi (X-Ray) hospitali ya Wilaya ikiwa ni pamoja na Ujenzi unaoendelea wa Kituo cha Afya Mikangaula unaogharimu milioni 200.

Chama cha Mapinduzi kupitia Mgombea mwenza kimeahidi kuwa ikiwa kitapata ridhaa ya kuongoza nchi kwa miaka mitano tena kitaendelea na sera yake ya Elimu bure ili kuhakikisha wanafunzi wanapata haki yao ya kimsingi ya Elimu.

Ifikapo 2023 Tanzania yote itakuwa na umeme, alisema Ndg. Samia Suluhu Hassani akizungumzia Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijiji ambao upo hatua ya tatu (REA III).

Akizungumzia suala la miundombinu ya barabara Mjini Mangaka, Ndg. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa ujenzi wa lami kilomita saba utatekelezwa. Aidha, Wakala wa barabara mijini na vijijini (TARULA) itaendelea kuongezewa bajeti ili kuimarisha miundombinu ya barabara.

Mgombea Ubunge Jimbo la Nanyumbu Ndg. Yahya Ally Mhata pamoja na wagombea udiwani wa Kata za Kilimanihewa na Mangaka kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi wameelezea namna Serikali inayosimamiwa na CCM ilivyotekeleza Miradi mikubwa Nanyumbu ukiwemo mradi mkubwa wa kimkati wa Ujenzi wa Stendi ya Kisasa ya Mabasi Mangaka unaogharimu Shilingi Bilioni 2.1. Aidha, Wagombea hao wameomba wananchi kuwachagua katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28/10/2020.    



Matangazo

  • Tangazo la Kazi za Muda za MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 May 06, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA NANYUMBU July 02, 2022
  • Ona yote

Habari Mpya

  • MWAKA MMOJA WA MKUU WA WILAYA NANYUMBU

    June 21, 2022
  • NANYUMBU KUTOA KIDATO CHA SITA kwa Mara ya Kwanza toka Uhuru

    May 06, 2022
  • Tumehitimisha MAADHIMISHO ya Muungano kwa Bonanza la NANYUMBU

    April 27, 2022
  • NANYUMBU YANUNUA LORI LA KIMKAKATI

    April 13, 2022
  • Ona yote

Video

Utalii wa ndani Nanyumbu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • miongozo

Tovuti Mashuhuri

  • Public Service Management
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Nanyumbu

    Anwani ya Posta: 246, Masasi

    Simu: 0232934112/3

    Simu za Mikononi:

    Barua Pepe: info@nanyumbudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2017 Nanyumbu Distict Council . All rights reserved.